Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Hawza, mwezi mtukufu wa Ramadhani ni fursa ya kipekee ya kunong’ona dua na kujikurubisha kwa Mwenyezi Mungu. Katika mwezi huu wenye nuru, jalada maalumu la “Machipuko ya Uja” likiambatana na sehemu za dua za Imamu Sajjad (a.s.) kutoka katika Sahifa al-Sajjadiyya, kwa ufafanuzi wa Hujjatul-Islam wal-Muslimin Seyyed Abdulrazzaq Pirdehghan, mtaalamu wa Sahifa Sajjadiyya, litakuwa mgeni wa meza zenu za futari enyi wasomi.
Kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa Rehema, Mwenye Kurehemu; Imamu Sajjad (a.s.) katika sehemu ya Dua ya 44 ya Sahifa Sajjadiyya anasema:
«وَالْحَمْدُ لِلَّهِ الَّذِی جَعَلَ مِنْ تِلْک السُّبُلِ شَهْرَهُ شَهْرَ رَمَضَانَ».
“Na sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu ambaye amefanya miongoni mwa njia hizo mwezi Wake, mwezi wa Ramadhani.”
Katika kifungu hiki, Imamu anamshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuufanya mwezi mtukufu wa Ramadhani kuwa miongoni mwa njia za kufikia ihsani Yake. Sifa ya kwanza anayoitaja Imamu kuhusu mwezi huu ni kwamba ni mwezi wa saumu; anasema:
«شَهْرَهُ شَهْرَ رَمَضَانَ، شَهْرَ الصِّیامِ،»
“Mwezi Wake, mwezi wa Ramadhani, mwezi wa saumu.”
Onyo hili linatufundisha kuwa, yeyote aliyepata tawfiki ya kuufikia mwezi huu kutoka kwa Mwenyezi Mungu, lakini hakufunga – iwe kwa kughafilika au kwa makusudi – hatastahili rehema na baraka za Kiungu ambazo Imamu anazitaja katika dua hiyo.
Kwa kawaida, wale wenye udhuru wa kisheria wana hukumu zao maalumu na wanapaswa kutekeleza wajibu wao, lakini wale wasio na udhuru na wanaoweza kufunga kisha wakaghafilika au wakaacha kwa makusudi, hawataingia katika rehema hizo za Kiungu.
Kimsingi, kufunga – iwe katika mwezi wa Ramadhani au miezi mingine – kumesisitizwa. Ali ibn Abi Talib (a.s.) katika mojawapo ya hotuba zake anabainisha sifa za Muumini na anasema:
«اولئک اخوانی الذاهبون فحقّ لنا أن نظماءإلیهم و أسفا علیهم و نعضّ الأیدی علی فراقهم».“Hao ni ndugu zangu waliotangulia; inastahiki kwetu kuwa na shauku nao na kuhuzunika kwa kutengana nao.”
Anabainisha kuwa, Muumini ni ndugu wa Muumini mwenzake na ana haki kubwa juu yetu, kiasi kwamba tunahuzunika kwa kutengana naye na tunatamani kukutana naye.
Lakini watu hawa wana sifa gani hadi kufikia daraja hilo? Katika muendelezo wake, anataja moja ya sifa zao: “Matumbo yaliyodhoofika kwa saumu,” yaani wale ambao athari za kufunga zinaonekana wazi katika nafsi zao.
Imran bin A’yan amepokea kutoka kwa Ja'far al-Sadiq (a.s.) riwaya ifuatayo:
حَدَّثَنَا عَلِیُّ بْنُ إِبْرَاهِیمَ بْنِ هَاشِمٍ، عَنْ أَبِیهِ، عَنْ إِسْمَاعِیلَ بْنِ مُهْرَانَ، عَنْ حُمَرَانَ بْنِ أَعْیَنَ، عَنْ أَبِی عَبْدِ اللَّهِ عَلَیْهِ السَّلَامُ قَالَ: «کَانَ عَلِیُّ بْنُ الحُسَیْنِ عَلَیْهِ السَّلَامُ قَاعِدًا فِی بَیْتِهِ إِذْ قَرَعَ قَوْمٌ عَلَیْهِمُ البَابَ، فَقَالَ: یَا جَارِیَةُ انْظُرِی مَنْ بِالبَابِ؟ فَقَالُوا: قَوْمٌ مِنْ شِیَعَتِکَ. فَوَثَبَ عَجْلَانَ حَتَّی کَادَ أَنْ یَقَعَ، فَلَمَّا فَتَحَ البَابَ وَنَظَرَ إِلَیْهِمْ رَجَعَ وَقَالَ: کَذَبُوا، فَأَیْنَ السِّمَتُ فِی الوُجُوهِ؟ أَیْنَ أَثَرُ العِبَادَةِ؟ أَیْنَ سِیمَاءُ السُّجُودِ؟ إِنَّمَا شِیَعُنَا یُعْرَفُونَ بِعِبَادَتِهِمْ وَشَعْثِهِمْ، قَدْ قَرَحَتِ العِبَادَةُ مِنْهُمُ الآنَافُ وَدَثَرَتِ الجِبَاهُ وَالمَسَاجِدُ، خَمَصَتِ البُطُونُ، ذَبَلَتِ الشُّفَهُ، قَدْ هَبَجَتِ العِبَادَةُ وُجُوهَهُمْ، وَأَخْلَقَ سَهْرَ اللَّیَالِی وَقَطَعَ الهَوَاجِرُ جُثُثَهُمْ، المُسَبِّحُونَ إِذَا سَکَتَ النَّاسُ، وَالمُصَلُّونَ إِذَا نَامَ النَّاسُ، وَالمَحْزُونُونَ إِذَا فَرِحَ النَّاسُ، یُعْرَفُونَ بِالزُّهْدِ، کَلَامُهُمْ الرَّحْمَةُ، وَتَشَاغُلُهُمْ بِالجَنَّةِ».Imamu Ja’far al-Sadiq (a.s.) amesema: Siku moja Ali bin Husayn (a.s.) alikuwa ameketi nyumbani kwake, ndipo kundi la watu wakagonga mlango. Akaambiwa: “Ni nani mlangoni?” Wakasema: “Ni kundi la Mashia wako.” Akasimama haraka kiasi cha kukaribia kuanguka. Alipofungua mlango na kuwaangalia, alirejea na kusema: “Wamedanganya! Basi ziko wapi alama katika nyuso zao? Iko wapi athari ya ibada? Ziko wapi dalili za kusujudu? Hakika Mashia wetu hutambuliwa kwa ibada yao na unyenyekevu wao; ibada imeacha athari katika pua zao, imechukua nyuso na sehemu za kusujudia; matumbo yao yamedhoofika, midomo yao imenyauka; ibada imeonekana katika nyuso zao; wanakesha usiku na miili yao wameitenga na starehe; wao hutukuza Mwenyezi Mungu watu wanaponyamaza; huswali watu wanapolala; huhuzunika watu wanapofurahi; hutambuliwa kwa zuhudi; maneno yao ni rehema na shuguli yao ni kuutafuta Pepo.”
Katika hadithi hii, Imamu anaonesha kuwa Mashia wa kweli hutambuliwa kwa ibada yao, kwa mwenendo wao wa kweli na wa ikhlasi, kwa athari za saumu katika midomo yao na udhaifu wa matumbo yao, na kwa alama nyinginezo zilizobainishwa katika sira ya Ahlul-Bayt (a.s.).
Hivyo basi, nasi tunapaswa kujichunga tusijitenge na sifa hizi za Mashia wa kweli, na tusije tukawa miongoni mwa wale wanaodai tu bila kuwa na vitendo, kama alivyoonya Imamu Ja’far al-Sadiq (a.s.). Ni lazima tuhakikishe kuwa, saumu na ibada zetu zinaonesha alama za kuwa Mashia wa kweli.
Riwaya hii ni sehemu ndogo tu ya mafundisho ya Ahlul-Bayt (a.s.) kuhusu sifa za Mashia, na inaonesha kuwa; miongoni mwa sifa hizo ni kuwa watu wa saumu na kufunga bila udhuru wala visingizio. Mwenyezi Mungu atupe tawfiki ya kutenda hayo sote.
Maarifa haya tunayawasilisha kwa heshima katika hadhara takatifu ya Imamu Sajjad (a.s.); Ewe Mwenyezi Mungu, mteremshie rehma Muhammad na Aali Muhammad na uharakishe faraja yao.
Maoni yako